Tangazo la Nafasi za Kazi – Halmashauri ya Wilaya ya Siha (10 Juni 2025)

Halmashauri ya Wilaya ya Siha inatangaza ajira kwa Watanzania wenye sifa za kujaza nafasi 9 za kazi, kufuatia kibali cha ajira kutoka Ofisi ya Rais – Utumishi wa Umma. Nafasi zilizotangazwa ni kwa ajili ya kada ya Udereva na Uhazili.


📌 Nafasi Zinazotangazwa

1. Dereva Daraja la II – Nafasi 5

Majukumu:

  • Kukagua gari kabla/baada ya safari
  • Kuwapeleka watumishi kwenye safari za kikazi
  • Kutunza log book, kufanya usafi wa gari, kufanya matengenezo madogo
  • Kusambaza nyaraka na kutekeleza maagizo ya msimamizi

Sifa:

  • Kidato cha Nne, leseni Daraja E/C, uzoefu wa mwaka 1 bila ajali
  • Cheti cha mafunzo ya udereva kutoka VETA au chuo kinachotambuliwa

Mshahara: Ngazi ya Serikali TGS B


2. Mwandishi Mwendesha Ofisi Daraja la II – Nafasi 4

Majukumu:

  • Kuchapa barua/nyaraka, kupokea wageni, kutunza miadi na ratiba
  • Kuweka kumbukumbu, kuandaa mahitaji ya ofisi, kupanga vikao
  • Kusambaza majalada na taarifa ofisini

Sifa:

  • Kidato cha Nne/Sita, Diploma au NTA Level 6 ya Uhazili
  • Ujuzi wa hatimkato (100 maneno kwa dakika), na matumizi ya kompyuta (Word, Excel, Email, Internet)

Mshahara: Ngazi ya Serikali TGS C


📬 Maelekezo ya Maombi

  • Waombaji wote wawe na umri usiozidi miaka 45
  • Vyeti vya elimu na taaluma viwe vimehakikiwa na Mwanasheria
  • Vyeti vya nje vihalalishwe na NECTA, TCU au NACTE
  • Hakutakubaliwa: Result slips, testimonials, provisional results
  • Mwisho wa kutuma maombi: 23 Juni 2025
  • Tuma maombi kupitia mfumo rasmi wa ajira:
    👉 https://portal.ajira.go.tz

Anuani:
Mkurugenzi Mtendaji (W),
Halmashauri ya Wilaya ya Siha,
S.L.P 129, Siha.

Ajira Portal, Ajira Portal News, Mabumbe

Leave a Reply