Tangazo la Nafasi za Kazi – Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia Mbeya (MUST) 10-06-2025

Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia Mbeya (MUST), kupitia kibali cha ajira kutoka kwa Katibu Mkuu Kiongozi cha tarehe 02/05/2025, kinakaribisha maombi ya kazi kutoka kwa Watanzania wenye sifa na uwezo wa kujaza nafasi mbalimbali za kazi kwa mwaka wa fedha 2024/2025. Ajira hizi ni kwa kada mbalimbali za kitaaluma na kitaalamu katika mazingira ya elimu ya juu ya kisayansi na kiteknolojia.

Nafasi Zinazotangazwa (Jumla: 42)

KadaIdadi ya Nafasi
Assistant Lecturer12
Tutorial Assistant8
Nursing Officer II2
Medical Doctor II1
Library Assistant II1
Laboratory Technician II7
Assistant Nursing Officer II2
Health Laboratory Technician II1
Laboratory Technologist II3
Planning Officer II1
Procurement and Supplies Officer II1
Assistant Supplies Officer II1
Clinical Officer II2

🧾 Sifa za Waombaji:

  • Waasomi waliomaliza shahada au stashahada zinazotambulika na TCU/NACTE/NBAA/NECTA kulingana na kada husika.
  • Lazima kuwa na uwezo wa kufundisha, kuchunguza, na kuchapisha tafiti kwa nafasi za Assistant Lecturer.
  • Umri: Si zaidi ya miaka 45 kwa kada zote isipokuwa watumishi wa Serikali waliopo.
  • Uwezo wa kutumia kompyuta kwa majukumu ya kila siku ni lazima.

📬 Maelekezo ya Maombi:

  • Maombi yatumwe kwa njia ya mtandao kupitia mfumo wa ajira wa UTUMISHI:
    👉 https://portal.ajira.go.tz
  • Mwisho wa kupokea maombi: 24 Juni 2025
  • Maombi yasiyoendana na masharti au yaliyowasilishwa nje ya muda hayatafanyiwa kazi.

🏢 Anwani ya Maombi:

Makamu wa Mkuu wa Chuo,
Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia Mbeya,
S.L.P. 131,
Mwanjelwa, Mbeya, Tanzania.

Ajira Portal, Ajira Portal News, Mabumbe

Leave a Reply